Kwa mujibu wa tovuti ya Muhit, mashindano hayo yanafanyika baada ya kufanikiwa mashindano mengine kama hayo ambayo yalifanyika nchini humo mwaka uliopita wa 2010. Mashindano hayo yanawajumuisha watu walio na umri tofauti watoto kwa wazee, wanaume kwa wanawake na wavulana kwa wasichana. Sheria za usomaji Qurani zitapaswa kuheshimiwa na kulindwa na washiriki wote wa mashindano hayo. Sherehe za kuhitimisha mashindano hayo zinatazamiwa kufanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo Amsterdam hapo siku ya Jumatatu tarehe 18 Aprili. 774470