IQNA

Mkutano wa Uchumi wa Kiislamu kufanyika Qatar

12:12 - April 16, 2011
Habari ID: 2106284
Mkutano wa masuala ya kifedha na uchumi wa Kiislamu umepangwa kufanyika mjini Doha Qatar tokea leo Jumamosi hadi Jumatatu tarehe 18 Aprili chini ya anwani ya 'Ustawi Endelevu na Uchumi Mpana katika Mtazamo wa Kiislamu.'
Kikao hicho cha siku tatu kimeandaliwa na Kituo cha Masuala ya Kifedha na Uchumi wa Kiislamu cha Chuo cha Utafiti wa Kiislamu cha Qatar QFIS, Taasisi ya Utafiti na Mafundisho ya Kiislamu IRTI Jumuiya ya Kimataifa ya Uchumi wa Kiislamu na Kituo cha Utafiti na Taaluma ya Takwimu, Uchumi na Masuala ya Kijamii cha Nchi za Kiislamu SESRIC. Mkutano huo unachunguza njia za kupunguza umasikini na kuimarisha uchumi katika nchi za Kiislamu. 774456
captcha