Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani CAIR linashirikiana na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ISESCO katika kuandaa kikao cha kuchunguza suala la kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu huko katika jimbo la California nchini Marekani.
Kwa mujibu wa tovuti ya Isesco, kikao hicho kimepangwa kufanyika tarehe 21 na 22 mwezi huu wa Aprili katika Chuo Kikuu cha Berkeley jimboni California. Washiriki wa kikao hicho mbali na kujadili suala la kuongezeka chuki dhidi ya Uislamu watajadili pia njia za kukabiliana na suala hilo. Wawakilishi wa ISESCO watashiriki katika kikao hicho. 774688