IQNA

Qurani imeteremshwa kwa wanaadamu wote

14:36 - April 19, 2011
Habari ID: 2108495
Qurani Tukufu imeteremshwa kwa ajili ya wanaadamu wote na kwa hivyo ili kila moja aweze kuisoma na kunufaika na madundisho yake; suala la tarjuma ya Qurani lina udharura mkubwa.
Haya yamesemwa na mtarjumi maarifu wa Qurani nchini Iran Bw. Mostafa Rahmandust.
Rahmandust ambaye pia ni malenga mashuhuri nchini Iran amefasiri Qurani tukufu kwa lugha ya Kifarsi. Amesema kila mwanaadamu anapaswa kupata fursa ya kuisoma Qurani kwa lugha yake ili aweze kuyafahamu mafundisho yake. Aidha amesema wale wanaotekeleza jukumu la kuandika tarjuma ya Qurani wanapaswa kuwa Na ujuzi wa mafundisho ya Kiisloamu.
775210
captcha