IQNA

Olimpiadi a Qurani kufanyika Iran

18:31 - April 20, 2011
Habari ID: 2109303
Washiriki zaidi ya 200 wanashindana katika Olimpiadi ya kwanza ya Qurani itakayoanza Aprili 26 katika mji wa Yazd kati mwa Iran.
Olimpiadi hiyo ni maalumu kwa wasomi, wanafunzi na wafanyakazi wa vitivo 14 vya Chuo Kikuu cha Sayansi za Qurani.
Baada ya kushiriki katika mtihani ulioandikwa, washiriki wanajitayarisha kwa ajili ya mtihan wa qiraa, hifdhi, tarjuma na tafsiri.
Chuo Kikuu cha Sayansi za Qurani kina matawi 14 kote Iran. Chuo hicho kinasimamiwa na Shirika la Waqfu la Iran na hutoa mafunzo yanayuhusiana na Nyanja mbali mbali za Qurani Tukufu.
777207
captcha