IQNA

Makabila ya Iraq kumfungulia mashtaka Kasisi Terry Jones

16:01 - May 08, 2011
Habari ID: 2118738
Makabila ya Iraq yanapanga kumfungulia mashtaka kasisi mwenye misimamo ya kupindukia mipaka wa Marekani Terry Jones kwa tuhuma za kufanya jinai ya kuchoma moto kitabu kitakatifu cha Qur'ani.
Mwakilishi wa makabila ya Iraq Basim al Hijami amesema makabila hayo yatafungua mashtaka dhidi ya kasisi wa Kimarekani Terry Jones kutokana na kitendo chake kiovu cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu.
Amesema wakuu wa makabila hayo ya Iraq wanafuatilia kwa karibu maudhui ya kufikishwa mahakamani kasisi huyo Mmarekani.
Basim al Hijami ameongeza kuwa watu wote wanaopenda kheri duniani wanapaswa kuelewa kwamba Qur'ani Tukufu na Uislamu ni anwani ya upendo, amani na usalama na kwamba madharau ya kasisi huyo wa Kimarekani yamewachukiza mno Waislamu kote duniani.
Hatua ya kasisi huyo ya kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu imelaaniwa na Waislamu kote duniani. 787403

captcha