Kongamano hilo linasimamiwa na Jumuiya ya Urafiki na Kuwaunga Mkono Wananchi wa Libya nchini Senegal kwa kushirikiana na jumuiya nyingine za Kiislamu.
Wasimamizi wa kongamano hilo la kitaifa pamoja na wanafikra, maulamaa wa Kiislamu, maimamu wa swala za jamaa na wataalamu wa masuala ya kisiasa wa Senegal watahutubia kongamano hilo kuhusu mapambano ya wananchi wa Libya, mauaji yanayofanywa na serikali ya Gaddafi dhidi ya wapinzani na taathira za machafuko Libya katika nchi nyingine za Kiafrika. 788780