Hayo ni kwa mujibu wa Hujjatul Islam Mahdi Taeb, mhadhiri wa chuo kikuu, alipokuwa akizungumza mjini Tehran katika kikao cha ‘Kuchunguza Mwamko wa Ulimwengu wa Kiislamu’.
Akiashiria mwamko wa wananchi wa Bahrain, amesema mwamko huo unashika kasi siku baada ya siku na hivyo kutikisa misingi ya tawala za kiimla za Aal Khalifa na Aal Saud.
Amegusia ushindi wa taifa la Iran dhidi ya utawala wa kifalme na kiimla wa Pahlavi mwaka 1979 na kusema , ‘Aal Khalifa na Aal Saud hawana nguvu zaidi ya Wapahlavi’.
Amemtaja Imam Khomeini MA kuwa kiongozi mkubwa ambaye alitoa muongozo wenye busara uliopelekea ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, mapinduzi ambayo sasa ni ilhamu kwa mwamko wa Kiislamu unaoshuhudiwa duniani.
Kikao cha ‘Kuchunguza Mwamko Katika Ulimwengu wa Kiislamu’ kimefanyika katika Chuo Kikuu cha Tehran.
788935