IQNA

Maandamano ya Walebanoni katika Siku ya Nakama

12:27 - May 15, 2011
Habari ID: 2122354
Maelfu ya Walebanoni leo Jumapili wanapanga kufanya maandamano makubwa katika miji tofauti ya nchi hiyo kwa mnasaba wa kuwadia mwaka wa 63 wa kukumbukwa Siku ya Nakama ambayo ni siku ya kubuniwa rasmi utawala haramu wa Israel uliopora na kukalia kwa mabavu ardhi za Wapalestina.
Kwa mujibu wa tovuti ya lebanonfiles, Walebanoni wapatao 50,000 wanatazamiwa kushiriki kwenye maandamano hayo.
Neeraj Sing Msemaji wa Kikosi cha Kulinda Amani Kusini mwa Lebanon UNIFIL amesema kikosi hicho kitashirikiana na jeshi la Lebanon katika kulinda amani na usalama wakati wa kufanyika maandamano hayo.
Waandaaji wa maandamano hayo wamesema kuwa huduma mbalimbali zitatolewa kwa washiriki. 791332
captcha