IQNA

Mnada wa kuwasaidia wananchi wa Bahrain wafanyika Qatif

13:33 - May 15, 2011
Habari ID: 2122407
Kundi moja la wasanii wa mkoa wenye Waislamu wengi wa madhehebu ya Shia wa Qatif nchini Saudi Arabia limefungua mnada wa kazi zao za kisanii katika mtandao wa Facebook kwa lengo la kusaidia wananchi wanaokandamizwa wa Bahrain.
Watayarishaji wa mnada huo wanasema kuwa mapato yake yatatumwa kwa wananchi wa Bahrain hususan wanaunzi wa vyuo vikuu waliopatwa na masaibu kutokana na matukio ya hivi karibuni nchini humo.
Wamewataka watu wote kushiriki katika mnada huo kwa kuweka bidhaa zao au kutoa msaada wa fedha kwa ajili ya wananchi wa Bahrain.
Hapo kabla pia wasanii wa Kisaudi Arabia walipiga mnada bidhaa zao katika mtandao wa Facebook na kutoa mapato yake kwa watu waliopatwa na maafa ya mafuriko wa Jeddah. 791209
captcha