Mwenyekiti wa kamati inayosimamia mashindano hayo Ibrahim Muhammad Bumalha amesema, mashindano hayo yataanza leo baada ya swala ya Magharibi katika msikiti wa Hassan al Sheikh katika mji wa Dubai.
Amesema kuwa kamati inaosimamia mashindano hayo imeweka televisheni kubwa katika msikiti wa Hassan al Sheikh ili kuwawezesha wanawake pia kufuatilia mashindano hayo.
Ahmad Saqar al Suwaidi ambaye ni miongoni mwa wanachama wa kamati inayosimamia mashindano hayo amesema wasomaji 552 walishiriki katika awamu ya kwanza ya mshindano haya na kwamba awamu ya mwsho inawashirikisha vijana na maimamu wa misikiti.
791791