Akizungumza katika hafla ya kutoa vyeti katika Taasisi ya Da'awah ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kiislamu cha Islamabad, amewapongeza waliofuzu na kusema: 'tunapaswa kufuata mafundisho ya Uislamu ili kukabailiana na changamoto zilizopo katika umma wa Waislamu".
Prof. Malik ameendelea kusema kuwa: 'tunapaswa kujiepusha na taasisi ambazo zinawapotosha Waislamu kupitia tafsiri mbovu ya ujumbe wa Qur'ani Tukufu.
Akizungumza katika kikao hicho Prof. Shahibzada Sajjid-ur-Rahman, mkurugenzi mkuu wa Chuo cha Da'awah cha Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kiislamu cha Islamabad amesema hii ni mara ya kwanza wanafunzi wa chuo hicho wanaosoma kwa njia ya posta kupata vyeti vya kuhitimu masomo.
794437