IQNA

Kongamano la Bidhaa Halali kufanyika Moscow

12:51 - May 21, 2011
Habari ID: 2124960
Kituo kikubwa zaidi cha maonyesho ya kimataifa nchini Russia 'Crocus Expo' kilichoko mjini Moscow kitakuwa mwenyeji wa Maonyesho ya Kimataifa ya Bidhaa Halali kuanzia Mei 26-28.
Walioalikwa kushiriki katika maonyesho hayo ni wafanya biashara wa Russia na kimataifa ambao wanazalisha vyakula kama vile, bidhaa za kitiba, marashi au manukato, vipodozi na vilevile wanaotoa huduma za utalii, kifedha, kibenki, uwekezaji na uchapishaji.
Bidhaa au huduma katika maonyesho hayo huwa tayari zimepata cheti cha Kiislamu cha 'Halal'.
Maonyesho hayo ni fursa kwa washiriki kubadilishana mawazo kuhusu sekta ya bidhaa na huduma halali duniani.
793768
captcha