IQNA

Mashindano ya taifa ya Qur'ani ya Malaysia kuanza Juni 13

18:19 - May 23, 2011
Habari ID: 2127273
Mashindano ya taifa ya Qur'ani ya Malaysia yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 13 hadi 17 Juni katika mji wa Kuching kwenye jimbo la Sarawak nchini Malaysia.
Shirika la habari la Malaysia Bernama limeripoti kuwa habari hiyo imetangazwa na Naibu Waziri wa Masuala ya Kiislamu wa nchi hiyo Daud Abdul Rahman ambaye ameongeza kuwa Waziri Mkuu wa Malaysia Najib Tun Abdul Razaq ndiye atakayefungua rasmi mashindano hayo.
Sherehe za ufunguzi wa mashindano hayo pia zitahudhuriwa na Waziri Mkuu wa jimbo la Sarawak Abang Muhammad Salahuddin. 797114
captcha