Mashindano hayo yatakayofanyika katika vitengo vitano kwa washiriki walio na umri wa chini ya miaka 25 yatachukua muda wa siku 6.
Washiriki wa mashindano hayo watachuana katika hifhi ya Qur'ani nzima huku wakichunga sheria za tajwidi na tartili na kufasiri juzuu ya 15 ya kitabu hicho kitakatifu, hifdhi ya Qur'ani nzima wakichunga sheria na kanuni za tajwidi na tartili, hifdhi ya juzuu 20 za mwanzo kwa kuchunga kanuni za tajwidi na tartili, hifdhi ya juzuu 10 za mwanzo wa Qur'ani kwa kuchunga sheria za tajwidi na tartili na hifdhi ya juzuu 6 zinazofuatana za Qur'ani kwa kuchunga sheria za tajwidi na tartili.
Marefa mashuhuri wa mashindano ya kimataifa ya Qur'ani watasimamia mashindano hayo na washindi watatangazwa mwishoni mwa mashindano.
Masharti ya washiriki wa mashindano hayo ni kuwa wasiwe ni wasomaji mashuhuri wa kimataifa, wahadhiri wa somo la tajwidi na tartili, washiriki katika duru zilizopita za masomo hayo wala wahitimu wa Chuo Kikuu cha al-Azhar. 796771