IQNA

Idara ya Masuala ya Qur'ani kuanzishwa katika Wizara ya Sheria ya Bahrain

18:36 - May 23, 2011
Habari ID: 2127286
Idara ya Masuala ya Qur'ani itaanzishwa hivi karibuni katika Wizara ya Sheria, Masuala ya Kiislamu na Wakfu ya Bahrain.
Idara hiyo itaanzishwa kwa amri ya Mfalme Hamad bin Isah Aal Khalifa wa nchi hiyo. Amri hiyo inatolewa katika hali ambayo askari jeshi wa nchi hiyo wakishirikiana na wa Saudi Arabia wamekuwa wakichoma moto Qur'ani Tukufu na kubomoa misikiti ya nchi hiyo. Utawala wa nchi hiyo haujachukua hatua yoyote ya kukabiliana na wahalifu.
Kwa kuzingatia mazingira ya hivi sasa ya Bahrain ambapo wapinzani wanakandamizwa na matukufu ya Kiislamu kuvunjiwa heshima kwa amri ya mfalme huyo, amri yake ya hivi sasa ya kuanzishwa idara ya Qur'ani katika wizara iliyotajwa inatambuliwa na wataalamu wa mambo kuwa ni hatua ya ujanja kwa madhumuni ya kuhadaa fikra za waliowengi na kufunika jinai za utawala huo za kuchoma moto Qur'ani na kubomoa misikiti ya Waislamu wa madhehebu ya Shia. 796772
captcha