IQNA

Kesi ya Mholanzi aliyevunjia heshima Qur'ani kuendelea

12:18 - May 25, 2011
Habari ID: 2128314
Mahakama ya Amsterdam nchini Uholanzi ilitangaza siku ya Jumatatu kuwa itaendelea na kesi dhidi ya Geert Wilders mbunge mwenye chuki na misimamo ya kibaguzi dhidi ya Uislamu na Waislamu na ambaye tayari ametengeneza filamu ya kuvunjia heshima matukufu ya Kiislamu kwa jina la Fitna.
Mahakama hiyo imetangaza kuwa kuna udharura wa kufuatiliwa kesi hiyo ambapo mbunge huyo amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuchochea vitendo vya ubaguzi dhidi ya Waislamu na kuukosea heshima Uislamu.
Jean Morris jaji anayeendesha kesi hiyo amekanusha madai ya Bram Moszkovicz wakili wa Wilders kwamba mahakama hiyo haiendeshi kesi hiyo kwa uadilifu.
Kesi hiyo ilianza mwezi Oktoba mwaka uliopita baada ya Waislamu na watu wenye misimamo ya wastani nchini Uholanzi kufikisha mahakamani mashtaka yao dhidi ya mbunge huyo aliye na uadui mkubwa na Uislamu. Miongoni mwa mashtaka yaliyowasilishwa mahakamani dhidi ya Wilders ni pamoja na ubaguzi wake dhidi ya Uislamu na Waislamu, kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu na utengenezaji wa filamu ya Fitna inayovunjia heshima matukufu ya Kiislamu.
Hivi karibuni mbunge huyo pia alitoa matamshi ya dharau na ubaguzi dhidi ya Waislamu alipokuwa akitoa mchango wake bungeni kuhusiana na suala la muundo wa Waislamu katika jamii ya Uholanzi. 797601
captcha