IQNA

Mkutano wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt AS wafanyika Kenya

14:53 - June 13, 2011
Habari ID: 2137047
Mkutano wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt AS umefanyika katika mji mkuu wa Kenya Nairobi kuanzia Juni 11 hadi 12.
Mkutano huo umewakutanisha viongozi wa Kishia kutoka nchi mbalimbali za Afrika.
Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu wafuasi wa madhehebu ya Ahlul Bayt.
Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt ni taasisi isiyo ya kiserikali yenye makao yake makuu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Lengo lake ni kueneza mafundisho ya Mtume Mtukufu wa Uislamu na Watu ya Nyumba yake yaani Ahlul Bayt kote duniani.
Kati ya waliohudhuria mkutano huo wa Nairobi ni kiongozi wa Mashia wa Nigeria Sheikh Ibrahim Zakzaki.
807305
captcha