IQNA

Walimu 500 kushiriki katika ustawishaji taaluma ya Qur'ani Iran

14:27 - June 13, 2011
Habari ID: 2137479
Walimu 500 wamefuzu kutoa mafunzo ya Qur'ani kwa walimu wa darasa la nne katika shule za msingi nchini Iran.
Mtaalamu wa Qur'ani anayeshughulikia uandishi vitabu katika Wizara ya Elimu ya Iran Bw. Reza Nabati amesema mpango maalumu ulianza kwa majaribio mwaka 2009 na sasa utatekelezwa kikamilifu mwaka huu.
Amesema waalimu wa Qur'ani 506 watakaotoa mafunzo hayo wamepita katika kozi maalumu ya kufunza Qur'ani katika shule za msingi. Amesema lengo la mafunzo hayo ni kuimarisha kiwango cha qiraa ya Qur'ani miongoni mwa wanafunzi wa darasa la nne na pia la tano.
807293
captcha