Sheikh Adam alikuwa akizungumza Juni 14 katika mji wa Kumasi kusini-kati mwa Ghana wakati wa semina ya ustawi wa vijana walio katika mwaka wa mwisho katika Shule ya Sekondari ya Sakafia.
Amesema kuna haja ya kutatua tatizo kubwa la ukosefu wa kazi, umasikini na kutojua kusoma katika jamii za Waislamu wa eneo hilo.
Sheikh Adam alisema sasa Waislamu wanapaswa kutoa kipaumbele kwa vizingiti vya ustawi wa vijana Waislamu katika zama hizi za utandawazi.
Amewataka vijana Waislamu nchini Ghana wawe wacha Mungu na wazingatie maadili ya kazi ili waweze kufanikiwa maishani.
Ghana ni nchi iliyo magharibi mwa Afrika yenye idadi ya watu takribani milioni 24 na Waislamu ni karibu asilimia 20 ya wakaazi wa nchi hiyo.
809990