IQNA

Iran yafungua kituo cha Darul Qur’ani nchini Sri Lanka

17:08 - July 02, 2011
Habari ID: 2147188
Kwa mnasaba wa siku ya Mab’ath tarehe 27 Rajab, Iran imefungua kituo cha Darul Qur'an katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo.
Sherehe za ufunguzi zimehudhuriwa na mkuu wa Idara ya Utamaduni ya Iran Mahdi Gholi Rokni na Balozi wa Iran nchini Sri Lanka Rahimi Gorji pamoja na wanazuoni wa Kiislamu nchini humo.
Kituo hicho ambacho kimefunguliwa baada ya kupata idhini ya Idara ya Masuala ya Waislamu nchini Sri Lanka kitakuwa na shughuli kadhaa zikiwemo za kiraa na kuhifadhi Qur’ani Tukufu. Kituo hicho pia kitaandaa mashindano ya Qur’ani.
Mkuu wa Idara ya Utamaduni ya Iran nchini Sri Lanka amesema kuna mpango wa kuanzisha Darul Qur’ani katika mji wenye Waislamu wengi wa Valechina.
818028

captcha