Kwa mujibu wa Dr. Hamad Bin Ali Sheikh Ahmad Al Sheibani, Mkurugenzi wa Idara Masuala ya Kiislamu na Utoaji Misaada ya Dubai amesema kuwa taasisi hiyo itatoa huduma maalumu katika uga wa Qur'ani na kuhifadhi Qur'ani.
Taasisi hiyo imefadhiliwa na Abdullah Al Abduli na inatoa huduma zake bila malipo.
Salah Abdurrahman Al Makhit ambaye anasimamia masuala ya Kiislamu katika Idara Masuala ya Kiislamu na Utoaji Misaada amesema idhini ya kuanzishwa taasisi hiyo imetolewa baada ya mfadhili wake kukutana na maafisa wa idara hiyo.
820502