Kwa mujibu wa Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu (ICRO) lenye makao yake mjini Tehran, hafla hiyo itafanyika Julai 7 baada ya Sala za Magharibi na Isha katika Hoteli ya Wairani mjini Harare.
Kati ya watakaotoa hotuba katika kikao hicho ni Abu Khalili Naibu Mkuu wa Jamii ya Walebanoni nchini Zimbabwe na Bw. Asadi Muwahhed, Mwambata wa Utamaduni wa Iran nchini Zimbabwe.
Mada za hotuba zitakuwa 'Kuzaliwa Imam Hussein AS kwa mtazamo wa Mtume Mtukufu SAW' na 'Historia ya minasaba ya Kiislamu kwa mujibu wa Qur'ani na Hadithi'.
820552