Kardinali Jean Louis Tauran amesema mazungumzo kati ya dini mbalimbali hayana maana ya viongozi wa dini tofauti kuketi pamoja na kuchukua uamuzi wa kuanzisha dini moja kwa ajili ya walimwengu wote bali mazungumzo hayo yanakusudia kutayarisha mazingira bora ya wafusi wa dini zote za Uislamu, Ukristo na Uyahidi kuishi pamoja kwa amani na utulivu.
Ameongeza kuwa wakati mwingine kunajitokeza ufahamu usiokuwa sahihi kwamba maana na mazungumzo kati ya dini tofauti ni kuchunguza hitilafu zilizopo kati ya dini tofauti na hata baadhi ya watu wanadhani kuwa viongozi wa dini mbalimbali wanataka kuanzisha dini moja kwa ajili ya walimwengu wote. Kardinali Jean Louis Tauran amesisitiza kuwa mazungumzo hayo hayafanani na mazungumzo ya kisiasa wala hayana lengo la kushusha chini dini moja na kuimarisha nyingine. 820260