IQNA

Saudia kuandaa kozi ya kuhifadhi Qur’ani kwa Wanawake

10:24 - July 09, 2011
Habari ID: 2150757
Kitengo cha wanawake katika Taasisi ya Kuhifadhi Qur’ani mjini Jeddah Saudi Arabia kimetangaza kwamba kitaanda kozi ya kuhifadhi Qur’ani maalumu kwa wanawake.
Kwa mujibu wa tovuti ya Bab, Fatima bin Umar Nasif, mkuu wa kitengo hicho amesema kozi hiyo imeandaliwa kwa lengo la kutoa mafunzo kwa kizazi cha Qur’ani na kuwahimiza wanawake kutumia likizo za msimu wa joto kujifunza Qur’ani Tukufu na kutekeleza mafundisho ya Qur’ani katika maisha yao ya kila siku.
Ataf Manasi mkuu wa kamati andalizi ya kozi hiyo amesema watakaoshiriki katika kozi hiyo ni wale ambao tayari wanaweza kusoma vizuri Qur’ani na ambao wanafahamu misingi ya tajwidi.
820967
captcha