IQNA

Warsha za falaki kufanyika katika maonyesho ya 19 ya Qur'ani Tehran

14:22 - July 12, 2011
Habari ID: 2153296
Warsha kuhusu falaki zitafanyika katika Maonyesho ya 19 ya Kimatafa ya Qur'ani Tukufu ya Tehran ambayo hufanyika katika mwezi mtukufu wa Qur'ani.
Mkuu wa kitengo cha falaki katika maonyesho hayo Hujjatul Islam Mohammad Taghdiri amesema maonyesho hayo yatajumuisha mada kama vile mwezi mwandamo, muelekeo wa kibla na kutizama nyota usiku.
Ameongeza kuwa kitengo hicho cha falaki kitasimamiwa na taasisi ya nujumi ya Haram ya Abdul Azim Hassani AS mjini Tehran .
Nujumi kwa watoto, kalenda ya Kiislamu, nyakati za sala za maeneo mbalimbali ya dunia ni kati ya programu za kitengo hicho.
Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yatafanyika katika Ukumbi wa Sala wa Imam Khomeini katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
824296
captcha