IQNA

Mashindano ya kitaifa ya Qur'ani kufanyika Kuwait

9:12 - July 14, 2011
Habari ID: 2154247
Awamu ya 15 ya Mashindano ya Kitaifa ya Qur'ani Kuwait itafanyika mwezi Oktoba, imetangaza Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu nchini humo.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Anba, mashindano hayo yatakuwa na vitengo vya Tajweed na Hifdhi na mwaka huu kaulimbiu ya mashindano hayo itakuwa 'Qur'ani yangu Imeniongoza'.
Abdul-Mohsen Al-Kharafi kutoka Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kiislamu amesisitiza kuwa mashindano ya Qur'ani yana nafasi muhimu katika kulea kizazi cha mahufadhi na maqarii wenye umahiri ambao wanaweza kuiwakilisha Kuwait katika mashindano ya kimataifa.
Aidha ametoa wito kwa washiriki kutumia fursa ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kujiimarisha kwa ajili ya mashindano.
Msikiti Mkuu wa Kuwat utakua mwenyeji wa mashindano hayo.
Washiriki pia wametakiwa kupata kijitabu cha hukumu za Tajweed kupitia tovuti ya www.awqaf.org/quran au taasisi zinazoshiriki katika uandilizi wa mashindano.
824327
captcha