IQNA

Umoja wa Kiislamu njia pekee ya kubaliana na changamoto

13:10 - July 16, 2011
Habari ID: 2155125
Ayatullah Muhammad Imami Kashani, khatibu wa sala ya Ijumaa iliyosaliwa jana mjini Tehran amesema kuwa, umoja na mshikamano ndio jibu sahihi na la pekee la changamoto na matatizo yanayoukabili ulimwengu wa Kiislamu.
Akihutubu katika Chuo Kikuu cha Tehran paliposaliwa sala hiyo, Ayatullah Kashani amesema, iwapo Waislamu wataondoa tofauti zao na kuwa na mshikamano, basi wataweza kukabiliana vizuri na changamoto zote zinazoukabili ulimwengu wa Kiislamu.
Khatibu wa sala ya Ijumaa ya Tehran amewaambia wananchi wa Iran kwamba, njia pekee ya kuzishinda hila na njama za maadui wa Mapinduzi ya Kiislamu ni kwa kumtii Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil Udhma Sayyid Ali Khamenei ambaye ndiye shina la amani la taifa hili.
826109
captcha