IQNA

Mahakama ya Uswisi yampiga faini Lüthard

15:47 - July 16, 2011
Habari ID: 2155273
Mahakama ya Uswisi imempiga faini kiongozi wa chama cha kisoshalisti cha PNOS nchini humo Dominic Lüthard kwa kupatikana na hatia ya kuchochea maandamano dhidi ya dini ya Kiislamu.
Baada ya kusikiliza mashtaka ya Jumuiya ya Kiislamu ya mji wa Langenthal dhidi ya kiongoni wa chama cha PNOS, mahakama ya Uswisi imempata na hatia Lüthard na kumhukumu kulipa faini ya franga 200.
Oktoba mwaka 2010 Dominic Lüthard alitoa tangazo akiwataka wakazi wa mji wa Langenthal kufanya maandamano dhidi ya kile alichodai ni mpango wa kuifanya nchi hiyo kuwa ya Kiislamu. Karibu watu 150 wanaopiga vita dini ya Kiislamu walioshinriki katika maandamano hayo na kushambulia Kituo cha Kiislamu cha mji huo. 826190
captcha