IQNA

Waislamu wa Luxembourg kuanza Ramadhani tarehe 1 Agosti

17:58 - July 18, 2011
Habari ID: 2155982
Baraza la Maimamu wa Jamaa wa Luxembourg limetangaza siku ya tarehe 1 Agosti kuwa ndiyo siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Taarifa iliyotolewa na Baraza la Maimamu wa Jamaa wa Luxembourg imesema kuwa mwezi mtukufu wa Ramadhani utaanza tarehe 1 Agosti na kumalizika tarehe 29 ya mwezi huo.
Imesisitiza imetangaza uamuzi huo kwa kutilia maanani mahesabu ya kisayansi na amri ya Baraza la Ulaya la Fatuwa na Uchunguzi wa Kiislamu ya udharura wa umoja na mshikamano katika kuainisha nyakati za sikukuu za Kiislamu.
Taarifa hiyo ya Baraza la Maimamu wa Jamaa wa Luxembourg imeongeza kuwa tarehe 31 Julai litatangaza rasmi kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani. 827170


captcha