IQNA

Mashindano ya Qur’ani ya wanawake Tehran

13:08 - July 19, 2011
Habari ID: 2156375
Mashindano ya tano ya Qur’ani ya wanawake wa mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Tehran yatafanyika Julai 21 na 23.
Mashindano hayo ya hifdhi na tarteel yanafanyika kwa himaya ya Taasisi ya Darul Qur’ani ya Imam Ali bin Abi Twalib AS.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, mashindano hayo ya siku tatu yatakuwa na vitengo viwili vya walio chini ya umri wa miaka 16 na walio juu ya umri wa miaka 16 katika Ukumbi wa Husseiniya Fatimiyun. Mashindano hayo yatajumuisha hifdhi ya juzuu moja, juzuu tano, juzuu 10, juzuu 20 na Qur’ani kamili.
Hadi sasa watu 700 wamejisajili kushiriki katika mashindano hayo.
827361
captcha