Kikao hicho kimeandaliwa na Taasisi ya Dar Al-Hadith Al-Hassania ya Rabat kwa ushirikiano na Kituo cha Tafsiri ya Qur'ani nchini humo. Wasomi na wataalamu kutoka nchi mbalimbali duniani wanatazamiwa kuhudhuria mkutano huo.
Kati ya mada zitakazojadiliwa ni pamoja na 'Balagha ya Qur'ani na Nadharia ya Tarjumi', 'Kuhifadhi Balagha Katika Tarjumi', 'Kutarjumi Balagha ya Qur'ani', 'Tarjumi ya Lugha Asili na Lugha Kusudiwa na Changamoto Zake' na 'Changamoto za Balagha ya Qur'ani' kati ya mada zinginezo.
831274