IQNA

Sheikh wa al Azhar:

Shia na Suni washirikiane katika kutetea Uislamu

15:33 - July 26, 2011
Habari ID: 2160422
Sheikh wa al Azhar nchini Misri Ahmad Tayyib amesisitiza juu ya udharura wa kuwepo ushirikiano kati ya Waislamu wa madhehebu za Shia na Suni kwa ajili ya kutetea na kulinda Uislamu kote duniani.
Sheikh Ahmad Tayyib ambaye jana alifanya mazungumzo na ujumbe wa maulamaa wa Kishia na Kisuni kutoka Lebanon amesisitiza juu ya udharura wa kulindwa umoja na mshikamano kati ya Shia na Suni.
Amesema wafuasi wa madhehebu mbalimbali ya Kiislamu wanapaswa kupiga hatua zaidi mbele katika njia ya ushindi wa Uislamu kwa kuimarisha maelewano, umoja na mshikamano wao.
Sheikh wa al Azhar amesisitiza kuwa umoja wa Kiislamu unawezekana kupitia njia ya kuheshimiana na kila upande kuukubali mwingine. Amesema kuwa kuwavunjia heshima Ahlulbait (as) na masahaba wa Mtume ni mstari mwekundu ambao haupaswi kuvukwa na yeyote na amewataka maulamaa wa Kishia na Kisuni kutoa fatuwa zinazoharamisha kuwavunjia heshima watukufu hao. 832005


captcha