Taarifa ya Al Azhar imeelezea matumaini kuwa hujuma hiyo itaimarisha azma ya Norway ya kueneza amani na usalama kwa watu wote wa Mashariki na Magharibi.
Mashambulizi ya Norway yaliyopelekea makumi ya watu kuuawa yanaendelea kulaani duniani.
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) pia imelaani hujuma za kigaidi nchini Norway.
Katibu Mkuu wa OIC Profesa Ekmeleddin Ihsanoglu amesema, ‘Kufuatia hujuma za kigaidi nchini Norway, tunatuma salamu zetu za rambirambi kwa familia za wahanga, serikali na wananchi wa nchi hii”.
Katibu Mkuu wa OIC emetoa wito wa kuendelezwa ushirikiano wa kimataifa katika kukabiliana na ugaidi.
832449