IQNA

Uturuki yaitisha kikao cha dharura cha OIC kujadili njaa Somalia

15:02 - August 06, 2011
Habari ID: 2165788
Waziri wa Mambo ya Uturuki ameelezea wasiwasi wake kuhusu baa la njaa barani Afrika na hasa Somalia na kwa kuzingatia hilo ametaka Jumuiya ya Ushirikiano ya Nchi za Kiislamu OIC iandae kikao cha dharura.
Ahmad Davutoglu Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki akizungumza na waandishi habari wa Uturuku amesema hali ya watu wa nchi kadhaa za Afrika ni ya kusikitisha. Ametaka OIC iitishe kikao kujadili njia za kutuma misaada nchini katika Pembe ya Afrika.
Davutoglu amesema amezungumza na Katibu Mkuu wa OIC Profesa Ekmaeleddin Ihsanoglu na kumtaka aitishe kikao cha dharura kujadili kadhia ya njaa Afrika. Amesema Uturuki inatuma ujumbe Ethiopa, Kenya na nchi kadhaa za Afrika kwa lengo la kuwasaidia wenye njaa. 837757
captcha