Shughuli za kituo hicho zitakuwa zikisimamiwa na Jumuiya ya Mazungumzo ya Kidini ya Silsila, ambayo itakuwa ikipanga ratiba, vikao na mazungumzo yote yatakayofanyika katika kituo hicho.
Waislamu na Wakristo wamefurahishwa mno na uzinduzi wa kituo hicho ambacho wanasema kitakuwa na nafasi muhimu katika kuandaa mazingira yanayofaa kwa ajili ya kuishi pamoja kwa amani wafuasi wa dini mbili hizo muhimu za mbinguni.
Kituo hicho kitazinduliwa rasmi tarehe 20 Septemba ambapo viongozi wa Kiislamu na Kikristo na vilevile wa serikali na makundi ya kijamii na kisiasa wa Ufilipino wamealikwa kushiriki. 849937