Mamluki wa dikteta mtoro wa Libya Muammar Gaddafi wamewanyonga baadhi ya wafungwa na kuua pia raia kadhaa wa Libya, baada ya wanamapinduzi wa nchi hiyo kuingia Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo wiki iliyopita na kuyaweka mikononi mwao karibu maeneo yote ya mji huo.
Sarah Leah Whitson mkuu wa watetezi wa haki za binadamu huko kaskazini mwa Afrika amesema, nyaraka zilizokusanywa hadi sasa zinaonyesha kuwa vikosi vya askari watiifu kwa utawala wa Gaddafi viliwaua raia wengi wakati wanamapinduzi walipoingia mjini Tripoli. Ripoti hiyo imeongeza kuwa viwiliwili vya watu 18 wakiwemo wawili ambao mikono yao ilikuwa imefungwa, vimegunduliwa katika kizuizi cha mto mmoja karibu na eneo la ngome ya Muammar Gaddafi ya Babul Aziziya.
Watu walioshuhudia wamewaeleza watetezi hao wa haki za binadamu kuwa watu hao waliuawa na vikosi vya askari wa Gaddafi.850836