IQNA

Biashara ya tiba halali yaenea Kenya

12:35 - September 08, 2011
Habari ID: 2183493
Baada ya kustawi huduma za banki za Kiislamu na vyakula halali nchini Kenya sasa biashara ya tiba halali imeanza kuenea nchini humo.
Kwa mujibu wa gazeti linalochapioshwa Kenya la Business Daily Africa, eneo lenye Waislamu wengi la Eastleigh mjini Nairobi lina hospitali, kliniki na duka za dawa zinazotoa huduma za tiba halali.
Katika hospitali au kliniki zinazotoa huduma halali, suala la vyakula na dawa linazingatiwa ili kuhakikisha kuwa misingi ya Kiislamu inafuatwa. Aidha vituo hivyo vya afya vimetenga vyumba maalumu kwa ajili ya Waislamu kusalia.
Hivi sasa kuna mpango wa kujenga hospitali mpya katika eneo hilo ambayo usanifu majengo wake utazingatia masuala mbalimbali ya Kiislamu.
856677
captcha