IQNA

Msaidizi wa dikteta wa Libya atiwa nguvuni Tunisia

13:52 - September 08, 2011
Habari ID: 2183573
Msaidizi wa kiongozi wa utawala unaosambaratika wa Libya Muammar Gaddafi, Al Khuwaildi al Hamidi alikamatwa jana katika uwanja wa ndege wa Tunisia akiwa pamoja na watu wa familia yake.
Ripoti zinasema kuwa al Hamid aliwasili nchini Niger Jumapili iliyopita akiwa pamoja na binamu yake diketa mtoro wa Libya Muammar Gaddafi Mansur Dho pamoja na washauri na wasaidizi wengine wa dkteta huyo. Hata hivyo inaonekana kuwa baadaye al Hamidi alielekea Tunisia na kutiwa nguvuni wakati anajaribu kuondoka tena nchini humo. 856977

captcha