Taarifa zinasema kuwa wapiganaji 23 wanaomuunga mkono Gaddafi wameuawa katika mapigano hayo na wengine 9 kutiwa mbaroni.
Wanamapinduzi ambao tayari wameulazimisha utawala wa Gaddafi kuondoka katika mji mkuu Tripoli, wameingia katika mji wa Bani Walid baada ya mazungumzo ya pande mbili ya kuepusha umwagaji damu kushindwa kuzaa matunda.
Mji huo wa kistratejia ni moja ya miji ambayo bado inadhibitiwa na wafuasi wa Gaddafi. Miji mingine ni Jufrah, Sabha na Sirte alikozaliwa Gaddafi. 857755