Msemaji wa Ikwanul Muslimeen Mahmoud Ghazlan amelalamikia vikali pendekezo la Waziri Mkuu wa Uturuki Rajab Tayyib Erdogan ambaye amewataka watu wa Misri waunde dola ya kisekula au isiyo ya kidini. Ikhwanul Muslimin imesema matamshi hayo ya Erdogan ni uingiliaji wa mambo ya ndani ya nchi hiyo.
Weledi wa mambo wanaamini kuwa matamshi ya Erdogan ni pigo kwa harakati ya Ikwanul Muslimin ambayo inataka kushriki katika uchaguzi ujao nchini Misri. 861687