IQNA

Jasusi wa Israel akiri kuhusika na mauaji ya Mughniya

15:27 - September 18, 2011
Habari ID: 2189249
Jasusi wa utawala haramu wa Israel amekiri kuhusika na mauaji ya kamanda mwandamizi wa Hizbullah Imad Mughniyah mwaka 2008.
Akizungumza kupitia Televisheni ya Kitaifa ya Syria jasusi huyo mwenye uraia wa Jordan na Palestina amesema aliusaidia utawala haramu wa Israel katika kumuua kamanda huyo wa ngazi za juu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon. Mughniya aliuawa shahidi mjini Damascus.
Aidha jasusi huyo amekiri kuwapa majasusi ya Israel habari kuhusu maeneo kadhaa ya kisiri nchini Syria.
Katika miezi ya hivi karibuni Syria imekuwa ikikumbwa na machafuko na serikali ya Damascus inasema majasusi wa kigeni wanatoa misaada kwa magenge ya watu wenye silaha wanaolenga raia. Hadi sasa watu 1,600 wameuawa katika machafuko hayo.
Syria imesema maafisa usalama wake wapatao 700 wameuawa katika mapigano na mgenge hayo ya kigeni ambayo aghalabu yanapata msaada wa utawala haramu wa Israel.
862765
captcha