IQNA

Mahala alipojificha Gaddafi pajulikana

19:18 - September 28, 2011
Habari ID: 2195237
Afisa mmoja wa kijeshi wa Libya amesema kuna uwezekano kwamba dikteta wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi amejificha katika mji wa Gadamis ulioko katika mipaka ya magharibi mwa Libya.
Hisham Abu Hijr amesema dikteta mtoro wa Libya amejificha katika mji wa Gadamis akilindwa na watu wa kabila la Touareg.
Amesema mji huo uko magharibi mwa Libya na kwamba Gaddafi anajificha katika watu wa kabila hilo.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa baada ya kushindwa na wanamapinduzi wa Libya, Muammar Gaddafi sasa anapoteza udhibiti hata wa ngome zake kuu kama mji wa Sirte na Bani Walid. 869358
captcha