IQNA

Mashirika ya misaada ya Uingereza yaupa msaada wa kifedha utawala wa Kizayuni

16:19 - October 08, 2011
Habari ID: 2199881
Ripoti za hivi karibuni zinasema kuwa mashirika 30 ya misaada ya Uingereza yameupa utawala haramu wa Israel msaada wa kifedha upatao pauni milioni moja za Uingereza katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Mashirika hayo yametoa msaada huo uli utumike katika ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi katika ardhi za Wapalestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Israel katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Shirika la Uungaji Mkono kwa Israel la Uingereza pekee, tokea mwaka 2007 hadi sasa limeutumia utawala huo haramu pauni laki tatu za Uingereza kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi.
Inasemekana kuwa, mbali na misaada ya kifedha kwa ujenzi wa vitongoji vilivyotajwa, shirika hilo pia limekuwa likifadhili mafunzo ya kijeshi kwa askari wa Israel, askari ambao wamekuwa wakihusika katika vitendo mbalimbali vya jinai na mauaji dhidi ya Wapalestina wasio na hatia. 873869
captcha