IQNA

Mbinu za kufundishia masomo ya kidini kuchunguzwa Imarati

8:33 - October 10, 2011
Habari ID: 2201938
Uchunguzi kuhusu mbinu zilizotumika katika zama za kale kufundishia mafunzo ya Kiislamu ili kuweza kunufaika nazo katika zama hizi zitachunguzwa katika tawi la Chuo Kikuu Huru cha Kiislamu cha Iran huko katika Umoja wa Falme za Kiarabu.
Kikao cha uchunguzi huo ambao umedhaminiwa kwa ushirikiano wa chuo kikuu kilichotajwa na Chuo Kikuu cha Oxford kitafanyika mwanzoni mwa mwaka ujao.
Lengo la kufanyika kikao hicho cha siku tatu ni kunufaika na mbinu za masomo zilizotumika katika zama za kale kwa lengo la kuboresha viwango vya masomo katika vyuo vikuu. Uimarishaji wa mawasiliano na ushirikiano wa Magharibi na mashariki kwa madhumuni ya kunyanyua viwango hivyo vya masomo ni malengo mengine yatakayofuatiliwa katika kikao hicho.
Wanafikra na wasomi walio na hamu ya kushiriki kwenye kikao hicho wana muda wa hadi kufikia tarehe 15 Novemba wawe wameshawasilisha makala zao kwa sekritarieti ya kikao hicho. 876079
captcha