IQNA

Duru za kimataifa zatakiwa kulinda turathi za Kiislamu huko Quds

18:42 - October 26, 2011
Habari ID: 2212488
Kundi moja la wataalamu wa mambo ya kale kutoka nchi tofauti za dunia limeuandikia barua Umoja wa Mataifa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la umoja huo UNESCO likitaka hatua za lazima zichukuliwe na taasisi mbili hizo za kimataifa kwa shabaha ya kukabiliana na hatua ya utawala haramu wa Israel ya kutaka kujenga jumba la makumbusho ya kale kwa jina la Tasamuh juu ya makaburi ya kale ya Ma'manu Allah katika mji mtakatifu wa Quds.
Kundi hilo linalojumuisha wataalamu 84 kutoka vyuo vikuu na taasisi za utafiti kutoka pembe zote za dunia limetaka juhudi za kimataifa zifanyike ili kuuzuia utawala huo kuendelea mbele na mipango ya kutaka kujenga jumba hilo kwenye makaburi ya Kiislamu ya Ma'manu Allah.
Kundi hilo pia limempelekea nakala ya barua hiyo meya wa utawala wa Kizayuni wa mji mtakatifu wa Quds likimtaka azuie ujenzi wa aina yoyote juu ya makaburi hayo ya kale na kuheshimu matukufu ya Waislamu.
Kundi hilo linasema kuwa ujenzi wa aina yoyote juu ya makabari hayo ya kihistoria ni mkasa wa kiutamaduni na kihistoria. Vilevile limetaka watu wanaoudhamini kifedha utawala wa Kizayuni wa Israel ili uendeleze mipango ya kuharibu makaburi hayo ya kale pia wawekewe mashinikizo ya kimataifa. 887684
captcha