IQNA

Kongamano kubwa la Hija kufanyika Makka

18:00 - October 29, 2011
Habari ID: 2213839
Kongamano kubwa la Hija limepangwa kufanyika katika mji mtakatifu wa Makka tarehe Mosi Novemba chini ya anwani ya 'Misafara ya Hija katika Turathi ya Kiislamu, Masomo na Ibra'.
Mkutano huo utahudhuriwa na Waziri wa Hija wa Saudi Arabia Fouad Abdul Salam na maulamaa kutoka nchi mbalimbali duniani.
Lengo la kongamano hilo limetajwa kuwa ni kubadilishana mawazo kuhusu jinsi ya kuarifisha zaidi utamaduni wa ibada hiyo ya kidini.
Katibu Mkuu wa kongamano hilo Hisham Balabbas amesema kuwa kongamano hilo kubwa la Hija hufanyika kila mwaka chini ya usimamizi wa Wizara ya Hija ya Saudia kwa lengo la kubainisha maana ya faradhi hiyo adhimu na katika kongamano hilo kunafanyika jitihada za kuwafahamisha Waislamu matunda na taathira za kiutamaduni za maulamaa wa Makka tangu zama za awali za Uislamu. 889215

captcha