Kwa sasa pazia hilo linatengenezwa katika kiwanda kinachoshona na kudarizi pazia la al Kaaba mjini Makka.
Mkuu wa karakana inayotengeneza pazia hilo Kamaluddin Sawadi amesema kuwa wataalamu kutoka maeneo yote ya Saudia wanashughulikia pazia hilo la al Kaaba katika karakana hiyo.
Amesema pazia hilo la al Kaaba linahitaji hariri na nyuzi nyingi zilizopakwa maji ya dhahabu na fedha. Ameongeza kuwa gharama za pazia la sasa la al Kaaba ni riale milioni 20 za Saudi Arabia. Amesema pazia hilo litawekwa juu ya al Kaaba tarehe 9 Dhulhija na lile la zamani litakwa vipande vipande ambavyo kwa kawaida hutolewa zawadi kwa shakhsia au jumuiya mashuhuri za Kiislamu. 891603