IQNA

Marekani inajaribu kuteka nyara mapinduzi ya Tunisia

15:39 - November 09, 2011
Habari ID: 2219605
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani ametoa wito wa kuimarishwa ushirikiano wa nchi yake na wanamapinduzi wa Kiislamu wa Tunisia ikiwa ni katika juhudi mpya za nchi hiyo ya Magharibi za kuteka nyara mapinduzi ya taifa hilo la Kiislamu.
Akizungumza hivi karibuni mbele ya Taassi ya Kitaifa ya Demokrasia nchini Marekani NDI, Waziri Hillary Clinton amedai kwamba serikali ya Washington iko tayari kushirikiana na Waislamu walioshinda uchaguzi wa hivi karibuni nchini Tunisia.
Katika kudumisha siasa za hadaa za serikali ya Washington, Clinton amesema kuwa fikra za makundi yote ya Kiislamu hazifanani na amekitaka chama cha an-Nahdha kilichoshinda uchaguzi kushirikiana na watu wanaopinga utawala wa kidini nchini humo na kwamba serikali ya Marekani itashirikiana na chama hicho iwapo kitatekeleza takwa hilo la Washington.
Huku akisema kuwa chama cha an-Nahdha kimeahidi kuheshimu uhuru wa kidini na haki za binadamu zikiwemo za wanawake, Clinton amedai kwamba kwa kawaida makundi ya Kiislamu duniani hushindwa kutekeleza vyema demokrasia.
Akiwalenga Waislamu kwa kejeli, amesema vyama vya Kiislamu vinapasa kuheshimu demokrasia, kujiepusha na vitendo vya mabavu, kuheshimu sheria, uhuru, haki za binadamu na kujiepusha kuchochea hisia za kidini. 894994
captcha