Shirika la habari la Nun limeripoti kuwa katika maandamano hayo mahujaji wa Bahrain wamesisitiza juu ya udharura wa kupinduliwa serikali ya Aal Khalifa na kutoa wito wa kudumishwa maandamano hadi utawala huo utakapong'olewa madarakani.
Wapinzani wa utawala wa Bahrain wanaendelea kufanya maandamano nchini humo na licha ya ukandamizaji mkubwa unaofanywa na jeshi la nchi hiyo likishirikiana na askari wa Saudi Arabia lakini wangali wanasisitiza juu ya kutimizwa matakwa yao.
Hadi sasa watu 45 wameuawa shahidi na mamia ya wengine kujeruhiwa katika harakati ya mapinduzi ya watu wa Bahrain. 895418